Changamoto za ukuaji na ujana



UTANGUILIZI
Malezi ya vijana duniani kote yamekuwa na changamoto zake kulingana na wakati tunaokuwa nao, na athari za madiliko ya kiuchumi na maendelelo makubwa kabisa ya sayansi na teknolojia ya mawasiliano, vijana kote duniani leo wanao utamaduni mmoja, namna wanavyovaa, aina ya vyakula wanavyopendelea, aina ya muziki wanaoupenda, njia za mawasiliano nk. Kwahiyo dunani kote vijana wanaongea lugha moja na wanaelewana, mitindo ya mavazi, muziki na njia za mawasiliano vinawaunganisha sana vijana wote wa mijini na wale wa vijijni, wa mataifa ya dunia ya tatu na yale ya dunia ya kwanza.
                                         
Changamoto kubwa kwa wazazi ni kwamba wao wanataka kuwaamulia vijana wao kila kitu kwasababu hawawaamini, jambo hili vijana nao hawalikubali, vijana wanataka kuwa huru, wanataka kuheshimiwa, kuthaminiwa, na kutambuliwa kama watu wazima; lakini pia vijana hawa wanatawaliwa na hofu wasiyoijua kuhusu kesho yao.

Wazazi wengi wanasahau kwamba kudai uhuru ni suala la asili la mwanadamu. Ndiyo maana ni rahisi sana kwa wazazi wengi leo kusikika wakisema “vijana wa siku hizi hawana adabu”, wanasahau kwamba hata wao walipokuwa vijana wazazi wao walisema vivyo hivyo juu yao, ni muhimu kutambua kwamba kila kizazi/zama kina watoto, vijana, na wazee, na majukumu yao pia ni tofauti kwahiyo kila kizazi kiana vijana wa siku hizi, watoto wa siku hizi, na wazee wa siku hizi.

Majukumu ya kizazi kimoja kwenda kingine ni lazima yawe tofauti, Rais wa awamu ya pili ndg A.Mwinyi alipata kusema maneno haya “kila zama na kitabu chake”

Pamoja na mengi kuhusu changamoto za vijana yaliyoelezwa katika chapisho hili, jambo kubwa la kuwahimiza na kuwatia nalo moyo vijana ni kuawashirikisha juu ya mpango mwema wa Mungu kuhusu maisha yao ya sasa na ya baadae. Yeremia 28:11-12.


A.  HATUA ZA UKUAJI WA MTOTO
OEDIPUS NA ELECTROPUS
Tafiti nyingi duniani kuhusu makuzi ya watoto zinaonesha kuwa watoto wanapofikia umri wa miaka 3-5 huwa wanaingia kwenye hatua inayoitwa kwa kitaalam PHALLIC STAGE, ambapo katika hatua hii mtoto wa kiume huwa anamtamani mama-OEDIPUS COMPLEX,  na mtoto wa kike anamtamani baba – ELECTRA COMPLEX.
Hatua za ukuaji wa mtoto zipo 5, na kila hatua ina kuwa na namna yake ambavyo mtoto anaifurahia kwenye mwili wake kadri anavyokuwa:-
      i.        Oral stage mwaka 0-1; katika hatua hii furaha ya mtoto inakuwa kwenye midomo yake, ndiyo maana utakuta kila anachokishika anapeleka mdomoni.

    ii.        Anul stage miaka1-3; katika hatua hii furaha ya mtoto inakuwa kwenye uume/uke, na kwenye njia ya haja kubwa, hapa mtoto anakuwa anajikojolea mara kwa mara na kujinyea, na kwa watoto wa kiume huwa wanapenda sana kuchezea uume wao. Ukiona mtoto anachezea uume wake usimkataze, unapomkataza madhara yake huwa ni kupungukiwa nguvu za kiume.

   iii.        Phallic stage miaka 3-5; ndiyo hiyo ya watoto kuwatamani wazazi wao kwa tofauti ya kijinsia

   iv.        Latency stage miaka 5-6; katika hatua hii mtoto anakuwa anapenda sana kufanya kazi za kiubunifu nyumbani, shuleni, kanisani nk.

    v.        Adolescent stage (first stage) miaka 7-11
Katika hatua ile ya 3, Phallic stage; Hali ile ya mtoto kumtamani mzazi huweza kuendelea kwa baadhi ya watu hadi wanapofikia umri wa balehe (puberty) ya mwisho miaka 12 – 19 kwa wasichana na miaka 14-18 kwa wavulana, na kwa wengine huendelea hadi wanapokuwa watu wazima kabisa. Hapa utakuta mama anapenda zaidi watoto wake wa kiume kuliko wakike, na baba anapenda zaidi watoto wake wakike kuliko wakiume, na huwa hamna sababu inayopimika ya upendeleo huu.
Katika hali hii kwa baadhi ya wasichana mara nyingi utakuta wanakuwa karibu zaidi na wavulana/wanaume kuliko wasichana/wanawake wenzao, na baadhi ya wavulana kuwa karibu zaidi na wasichana/wanawake kuliko wavulana/wanaume wenzao; hii huwa haijalishi ni eneo gani wapo, wakiwa shuleni, wakiwa kanisani, wanapokuwa kambi, nk. Siyo kwamba wanakuwa hawana upendo na wenzao wa jinsia sawa na wao, hapana ni kwavile wanakuwa wanajisikia kuwa huru zaidi wanapokuwa na mtu/watu wa jinsia tofauti na ya kwake, huwa wanakuwa huru sana kiwango cha kuwaambia na kuwashirikisha hisia na mambo yao ya ndani sana kuhusu mahusiano yao na wapenzi wao, mahusiano yao na wazazi/walezi wao, mahusiano yao na waalimu wao, wachungaji wao, na mahusiano baina yao na ndugu zao nyumbani.
Katika Biblia upo mfano wa Yakobo, yeye alikuwa anajisikia huru zaidi kwa mama yake kuliko ilivyokuwa kwa baba yake, Mwanzo 25:28.
Kiujumla vijana wengi (12-19)wanapokuwa wamefikia umri wa balehe na umri wa kuzidi (19+), wanakuwa na machaguzi mengi juu ya maisha yao, na hii inatokana na maswali mengi ya hofu wanayokuwa nayo kuhusu maisha na hali yao ya baadae, na wanapenda kuwa huru na maisha yao, wanapenda kuona wanathaminiwa na kupendwa. Katika mazingira haya hujikuta wanakuwa wachaguzi wa watu wa kuzungumza nao ambao huwa wanahisi kuwa hao ni watu wano waelewa zaidi ya mtu mwingine yeyote hata wazazi wao, wapo vijana ambao wapo huru na karibu zaidi kwa watu wa nje zaidi ya walivyo huru kwa wazazi wao na ndugu zao nyumbani. Lakini hii pia inachangiwa na baadhi ya wazazi ambao huwachukulia watoto wao kwa mazoea.
Wazazi na waalimu mara nyingi hawapendi kuwapa watoto/vijana uhuru wanaoutaka kwakudhani kuwa kufanya hivyo ni kuwadekeza na kuwapoteza, kinachotokea vijana wanaponyimwa uhuru na heshima wanayoitaka ni mgogoro kati ya wazazi na vijana wao kwa upande mmoja, na waalimu na wanafunzi wao kwa upande mwingine, kwasababu vijana wataendelea kudai uhuru wao hadi waupate; mfn wa Yesu Lk 2:41-49, na mwanapotevu Lk 15:11ff.
Mara nyingi vijana wanalaumiwa na wazazi na waalimu wao kuwa wanakiburi, lakini kumbe wakati mwingine hiyo ndiyo njia yao kujitetea na kudai na uhuru, tunawaona wana kiburi kwasababu mara zote tunataka wafanye kama tunavyotaka sisi na kwa njia zetu bila kuwaachia na wao watumie njia wanayoweza kuitumia kufanikisha jambo lilelile.
Ni muhimu kuwaelewa, na kuwapa uhuru wao, hii itawasaidia wazazi/walimu kujua uwezo walionao watoto na wanafunzi wao juu ya masuala fulanifulani ya kimaisha. Wajibu wetu wazazi na waalimu ni kuwasaidia vijana wakue kufikia kuwa watu wazima wanaoujua wajibu wao na wanaojitosheleza, wanapofanya jambo wakalikosea na pengine kuwaumiza wao wenyewe, wakati mwingine watalifanya jambo hilo kwa umakini zaidi ili kuepusha madhara kwao na kwa wengine, na huo ndiyo uwajibikaji wenyewe.
Tukitaka kufaulu katika hili ni muhimu sana kujenga juu ya msingi wa mawazo na maoni waliyonayo vijana kuliko kuwataka wao wajenge juu ya msingi wa hoja na maagizo yetu wakati wote. Ukali na vitisho kwa watoto/vijana ni dalili ya kushindwa malezi.
Mwalimu kuwa zaidi ya mwalimu; mzazi kuwa zaidi ya mzazi, kuwa menta.
Menta:
Huyu ni mtu mwenye ujuzi, uelewa mpana na uzoefu katika masuala fulanifulani ya kimaisha, biashara, kilimo, huduma, na kazi. Wajibu mkubwa wa menta ni kuwaongoza wengine kufikia matarajio yao. Menta ni mshauri, ni mwezeshaji, ni kiongozi.
Vijana ni umri wa kipekee sana, vijana sio watoto na wala si watu wazima, hawapendi kuwa watoto bali wanatamani kuwa watu wazima, na bahati mbaya sana hawajui namna gani wafanye ili wawe watu wazima, na watu wawatambue hivyo, hapa ndipo inabidi mzazi asiwe mzazi tu na mwalimu asiwe mwalimu tu, wawe menta.
Sifa za menta:
        i.        Utayari wa kuwashirikisha wengine maarifa na ujuzi alionao pasipo kuwabagua jinsia, kabila nk.
       ii.        Rafiki
      iii.        Mwenye kusikiliza zaidi ya anavyoongea
      iv.        Mwenye mtazamo chanya kimaisha kwake mwenyewe na kwa anaowaongoza
       v.        Kujidhabihu kwaajili ya wengine
      vi.        Mwenye uwezo mkubwa katika kujieleza na mawasiliano
    vii.        Mwenye kufurahia kufanya anachokifanya
   viii.        Mwenye kujiendeleza kupata maarifa mapya
      ix.        Mwenye uwezo wa kutatua migogoro
       x.        Anayejiamini
      xi.        Mwenye kuheshimu mawazo na mitazamo ya wengine na kukubali jitihada zinazofanywa na wengine
    xii.        Mkweli na mwenye kutimiza ahadi
   xiii.        Anayeza kujifunza kutoka kwa wengine (si mjuaji wa kila kitu)
Hizi sifa zote, wazazi na waalimu wote wa vijana wanapaswa kuwa nazo, tukiwa nazo watoto/vijana, na hata watu wazima watatufuata wao wenyewe pasipo kulazimishwa na mtu. Unafuatwa na mtu kuombwa ushauri ama muongozo, tumia nafasi hiyo kikamilifu kumfanya huyo kuwa mwanafunzi wa Yesu.




               

               KUFANYA NA VIJANA
Anza na yale yenye kuleta matokeo hasi
Michezo kwenye mazingira rafiki
Tumia nguvu ya ubunifu
Washughulishe kwenye mambo makubwa ya kuleta heshima
Uwe mkweli, ndiyo yako iwe ndiyo na hapana yako iwe hapana; kataa ama kubali ukionesha heshima
Kusikiliza ni kipaumbele
Wekeza katika nguvu za vijana
Usiwafanyie, fanya pamoja nao


B.   KUWAJENGEA VIJANA UWEZO
Tunahitajika kuwajengea vijana uwezo kwa kuanza na vitu, mtazamo, karama, ujuzi, na hatua waliyonayo kwa kwakati huo. Kuwajengea uwezo ni suala la muhimu sana kwakuwa itawasaidia kujiamini , kujiheshimu na kuondoa ile hofu wanayokuwa nayo juu ya wakati ujao, kuhusu ajira, mahusiano, hali yao ya kiroho, uchumi nk.
Tunapowajengea uwezo vijana, kwenye suala la ajira, ni muhimu sana kuwapanua mawazo ili kwamba wanapotazama soko la ajira waone kuwa ni kitu wanachoweza kuanzisha wenyewe mmoja mmoja ama kwa kujiunga kwenye vikundi kwamaana ya kujiajiri wenyewe na kuajiri wengine. Tangu zamani za ukoloni vijana wengi waliopelekwa shuleni walikuwa wanasisitizwa na wazazi na waalimu juu ya kusoma kwa bidii wapate alama nzuri ili wapate ajira nzuri serikalini na kwenye makampuni, mtazamo huu umeendelea kuwepo hadi sasa kwenye jamii nyingi nchini mwetu, na Afrika.  Wapo wazazi wanaowahiza vijana wao wasome kwa bidii wapate alama nzuri ili waajiriwe, kwa hiyo vijana walio wengi sana wanawaza kuajiriwa tu.
Asilimia 70 ya vijana wenye miaka kati ya 13 na 34 ambao ndiyo wengi zaidi kati ya idadi ya watu milioni 45 waliopo Tanzani ni kundi kubwa ambalo ni tegemezi na hawana ajira. Hii ni kati ya nguvu kazi ya vijana milioni mbili na nusu amabo wako mijini na hawana kazi.
Hivi sasa vijana zaidi ya 30,000 wanahitimu katika vyuo mbalimbali na wengi wakiishia mitaani kwa kukosa ajira. Sasa hawa ni wa vyuo, wapo wengine walioshia darasa la saba, wapo walioishia kidato cha nne na sita, na kuishia huko huko mitaani huku wakiwa hawana ujuzi wowote.
Kutegemea kuajiriwa kwa sababu zozote zile sio kitu kibaya, lakini pia kutegemea kuajiriwa kwasababu yeyote ile ni kubaya. Mawazo ya kutegemea kuajiriwa siyo mawazo yenye afya sana na inafaa yafutwe kwa vijana na miongoni mwa wanajamii tulionao, wapo vijana wengi mtaani ambao wamechanganyikiwa na hawajui la kufanya kwakuwa soko la ajira ni gumu sana, hivyo wengi wamejiingiza kwenye vitendo hatarishi, kama ukahaba, matumizi ya madawa ya kulevya, uhalifu, nk.
Nukuu:
Kama yai livunjika kutokana na nguvu za nje huharibika, kama yai livunjika kutokana na nguvu zitokazo ndani maisha huendelea; mambo makubwa hutokea kuanzia ndani ya mtu na siyo nje.

C.  MUDA/WAKATI (time management)
Ni muhimu sana watoto na vijana wakawa na uelewa mkubwa kuhusu namna ya kutumia muda vizuri  (kuukomboa wakati)katika kufanikisha malengo ya maisha ya kila siku pamoja na kuziishi  ndoto za maisha yao. Ni lazima wafunzwe kanuni/mbinu za kuukomboa wakati.
Kila mtu anaishi ndani ya masaa 24, hakuna mtu mkwenye muda wake zaidi ya huo, sote tuna masaa sawa ya mchana, na masaa sawa ya usiku. Kutumia muda vizuri inamaanisha kuamua ni namna gani uantumia muda ulionao kupata unachokitataka, kutumia muda vizuri haimaanishi kuwa bize wakati wote. “Muda ni zawadi kutoka kwa Mungu na katu haiwezekani kuurudisha nyuma ukipita” – David and Janet Cunningham
Lengo kubwa la kujifunza namna ya kutumia muda vizuri ni ili kuongeza ufanisi na uzalishaji.
Matumizi sahihi/mazuri ya muda husaidia:-
      i.        Kuongeza utulivu
    ii.        Kupunguza msongo wa mawazo
   iii.        Kuridhika/kujiridhisha
   iv.        kupumzika
kanuni za kutumia muda vizuri:
      i.        Mpango kazi: “kupanga ni kuchagua”, “kushindwa kupanga ni kupanga kushindwa”; unaweza kutumia muda mwingi kuweka mpango kazi wa siku, mwezi, kota, mwaka, nk. Lakini hiyo itakusaidia kukamilisha majukumu yako kwa ufanisi. Mpango kazi ni muhimu ukawa na muda/saa, shughuli, ikibidi na muhusika, mfano
9:00asubuhi – 11:00asubuhi   chai
11:00asubuhi – 12:00mchana  kujisomea kitabu

    ii.        Nidhamu ya muda: panga mpango kazi na kasha ufanyie kazi mpango huo, usipoutekeleza mpango wako ni bure.

   iii.        Kuweka vipaumbele:- Unapokuwa na mambo mengi ya kufanya na unataka kuyafanya yote kwa pamoja, hautaweza hadi utakapoyagawa mambo yako katika vipande vidogo vidogo kutoka na umuhimu wake (importance) na uharaka wake(urgency). Unapoweka vipaumbele inajkusaidia kuanza na mambo yenye kuhitaji uharaka na yale ya muhimu.
Mtalaam wa masuala ya uchumi na soshologia Vifredo Pareto kwenye kanuni yake ya 80/20 anasema kuwa 80% ya matokeo yanayopatikana inatokana na 20% ya kazi iliyofanyika. Hii inamaanisha kwamba mtu anapokuwa na mambo kumi(10) ya kufanya, atarajie mafanikio kwa 80% kwa kutekeleza mambo mawili(2) tu ya muhimu kati ya hayo kumi.

   iv.        Sema hapana: Haiwezekani ukafanya kila kazi, unapokuwa umepanga mambo yako kuyafanya akatokea mtu mwingine na kukuingizia ratiba/jambo lake sema hapana.

    v.        Jitenge na vipoteza muda: vitu hivi ni  vitu muhimu kwenye maisha yetu lakini kwakweli hutupotezea sana muda, mfn utazamaji wa TV usio na mpango/uliopitiliza, maongezi yasiyo na faida, vikao visivyo vya muhimu, wageni wasio na mpangilio, simu na meseji, kuahirisha ahirisha mambo, kuendekeza usingizi, kutafuta vitu usivyokuwa na uhakika wapi vipo, kusubiria huduma unayoweza kuipata mahali pengine. Hapa unaweza kuwaachi vijana nao waeleze ni mambo gani yanayowapotezea muda.

   vi.        Kasimisha(delegating): Unapompa mtu mwingine wajibu wa kufanya majukumu yako huku ndiyo kukasimisha. Unapokasimisha madaraka ni muhimu kuchagua mtu mwenye uwezo kufanya ambavyo ungefanya wewe.

  vii.        Malengo: Ni lazima kujiwekea malengo ya namna utakavyo ikamilisha kazi yako, na kichwani uwe na picha kamili (picturise)ya namna kazi itakavyokuwa. Unaweza kupanga malengo ya muda mfupi nay a muda mrefu.

BI. MGAWANYO WA SHUGHULI KULINGANA NA UMRI NA MUDA TULIONAO
ZABURI 90:10
Siku za miaka yetu ni miaka 70, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini; Na kiburi chake ni taabu na ubatili, maana chapita upesi.
      i.        Umri wa kukua 0-25
    ii.        Umri wa mazalisho 25-60
   iii.        Umri wa kupumzika na kula matunda ya kazi yako duniani 60-70
   iv.        Kuishi paradiso kuanzia miaka 70

B2. MAISHA YETU KAMA SAA
§  Miaka 70 ndani ya masaa 24
§  Miaka 20=11asubuhi;
§  Miaka 25 = 12 mchana
§  Miaka 30 = 1 mchana
§  Miaka 35 = 2 mchana
§  Miaka 40 = 4 jioni
§  Miaka 45 = 5 jioni
§  Miaka 50 = 6 jioni
§  Miaka 55 = 8 usiku
§  Miaka 60 = 10 usiku
§  Miaka 70 = 12 usiku


Pamoja na kwamba tunao muda sawa, bado watu husema na kulalamika kuwa “muda hautoshi”
Basi utujulishe kuzihesabu siku zetu, tujipatie moyo wa hekima. Zaburi 90:12

















Lazaro JP Kavageme,
Founder, Inuka Tuondoke Ministries
Project Director at Child Development Center TZ 555
Mob:0787-654724/0769-085178
Inukatuondoke.blogspot.com

Jan 2017