Upo mchakato unaendelea, subiri.

 



Kuna kitu fulani unafanya, kuna maombi fulani unayaomba na unatamani kuona matokeo yake sasa na hayaonekani; usiche, endelea, na endelea kukiri uwepo wa matokeo japo hayaonekani; kuna mchakato unaendelea usiouona utakaoleta majibu ya maombi yako, utakaoleta heshima unayoistahili.

Tunajifunza kwa Yoshua kwa habari ya kukiri uwepo wa matokeo hata kama hayaonekani sasa, Yoshua alinena maneno ambayo yalikuja kitimia baada ya miaka takribani 600 baadae; Yoshua 6:26 maneno haya ni ya Yoshua wakati Israel wanaingia Kanaan, yakaja kutimia wakati wa Wafalme wa Israel, Wafalme wa kwanza 16:34

Tunajifunza kutoka kwa Daniel aliyeomba kwa muda wa siku 21 ndipo akapokea majibu yake, wakati anaomba kuna mchakato ulikua unaendelea, majibu ya maombi ya Daniel yalikuwepo tangu siku ya kwanza ya maombi; Malaika mwenye majibu ya maombi ya Daniel alikuwa anapambana na mkuu wa anga la Uajemi ili amfikiahie Daniel majibu yake, laiti kama Daniel angelikata tamaa asingelipokea majibu ya maombi yake na kumbe mchakato ulikuwa unaendelea. Daniel 10:12

Tunajifunza kwa mti wa Moso(bamboo) hurefuka hadi kufikia mita 27 ndani ya wiki sita tu na hapo ndipo huwa umekomaa tayari kwa kuvunwa, mmea wake baada ya kuchipuka huwa unakua kwa futi moja na nusu hadi mbili kwa siku, lakini kabla ya kuchipuka mbegu ya Moso hukaa ardhini kwa miaka mitano, ndiyo, miaka mitano. Kuchipuka na kukua kwa haraka kwa mti huu ni kwasababu ya kujiimarisha ardhini kwa muda wa miaka mitano, (mchakato).

Kuna mchakato usiouona unaendelea, jiamini katika hicho unachokifanya, muamini na umtumaini Mungu, kisha kiri kana kwamba imekwishakufanyika. Usikiri unachokiona sasa bali kiri kile usichokiona kana kwamba unakiona sasa, Warumi 4:17.