Kuishinda nguvu ya dhambi


Biblia inasemaje kuhusu namna tunavyoweza kuishinda hali na asili yetu ya dhambi na matamanio ya mwili? Jawabu ni kwamba ili kuondokana na kuishinda hali hii kuna jambo ni lazima tuache kulifanya na lipo tunalopaswa kuanza kulifanya mara moja, lakini hii itawezekana tukiwezeshwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kutufanya tuache matendo maovu na kutenda matendo mema.
Yesu alisema, pepo mchafu amtokapo mtu hutafuta mahali pa kukaa, akikosa huamua kurudi kule likotolewa, akikuta pako wazi huingia tena humo pamoja na marafiki zake. Mathayo 12:43-45.

Mwanafalsafa Mgiriki wa kale Aristotle Nicomachus, katika moja ya tafiti zake kuhusu fizikia ya horror vacui, yaani hofu ya OMBWE (uwazi wa kitu, tupu), alihitimisha kwa kusema "asili huchukia ombwe-nature abhors a vacuum; natura abhorret a vacuo. Kwamba kani/nguvu mzunguko za asili katika ulimwengu hutaka kujaza kila mahali panapokuwa wazi.

Unapoacha kufanya jambo/tabia fulani kwenye maisha yako, tafadhali haraka sana anza jambo/tabia nyingine mbadala, lisibaki ombwe vinginevyo zile kani mzunguko zinazochukia ombwe zitakuwekea tabia/jambo lake jipya ama kukurudishia tabia ileile uliyoiacha.
Hali ya kuwa na ombwe humkosesha mtu utulivu, humpa mahangaiko mengi hadi pale ombwe litakapozibwa (mke wa Potifa, sexual urge, Mwz 39:1-16); hata lile jambo linaloachwa nalo huhangaika kutafuta mahali palipo wazi likae, sasa linapokosa mahali pa kukaa, huamua kurudi kulekule lilipotoka na huingia hapo tena ikiwa patakuwa wazi.

Unapoamua kuacha tabia fulani isiyofaa, mfn ulevi, wizi, tamaa nk, anza tabia nyingine mpya inayofaa (Zbr 34:14, Ef 4:28), la sivyo ile tabia uliyoiacha itarudi tena.
Watu wengi hurudia tabia walizoziacha kwasababu ya kutokuanza tabia nyingine mbadala. Kuacha tabia zisizofaa pasipo kuanza tabia mpya haitoshi, hadi umeanza tabia mpya.(2Tim 2:22)

Barikiwa!

Acknowledgement: Biblical Christianity in African Perspective pg 203