Kwanini kujikunyata?!



Kwanini kujikunyata?!


Jinsi unavyojiona na kujisikia ni matokeo ya mtazamo ulionao. Unaweza kubadilisha hali mbaya uliyonayo kwa kubadilisha mtazamo wako tu. Mtazamo huamua hali ya mtu na pia hugeuka sababu ya vile alivyo.

Mtazamo wa mtu kuhusu utajiri/umasikini ndiyo sababu ya utajiri/umasikini wake; mtazamo wa mtu kuhusu uchawi ndiyo sababu ya uchawi wake; mtazamo wa mtu kuhusu uchawi ndiyo sababu ya kurogwa/kutorogeka kwake; mtazamo wa mtu kuhusu mke/mume wake ndiyo sababu ya jinsi anavyomchukulia; kufaulu/kufeli kwa mtu ni matokeo ya mtazamo wa mtu kuhusu mtihani wenyewe.

Mtazamo wa mtu kwa kawaida huwa chanya ama huwa hasi; kwa bahati mbaya sana watu wengi wanaanguikia katika kundi la watu wenye mitazamo hasi juu ya maisha yao, anapopatwa na jambo baya hujitazama yeye mwenyewe kuwa ndiyo sababu ya jambo hilo (vitu kama kulaaniwa, mkosi, bahati mbaya nk)ama hutafuta mtu/watu fulani kuwa ndiyo sababu ya kutokea kwa jambo hilo; mtu hasi huchukulia jambo baya ama tatizo kama kitu cha kumkwamisha kufikia jambo fulani badala ya kuona kikwazo/jambo hilo kama fursa ili atende kwa ubora zaidi.

Vile ulivyo ni mtazamo wako. 
Rafiki yako,
Lazaro JP Kavageme 
0769-085178/0787-654724