FANYA, FANYA, FANYA………...

Screenshot_2015-10-16-09-37-05
Fanya kitu ambacho ni muhimu kwako kukifanya,
Fanya ikiwa muda wa kukifanya hicho unachotaka kukifanya umewadia,
Fanya pasipo kutaka kuwavutia watu,
Fanya pasipo kuwa na hofu ya kushindwa na kuchekwa mbeleni ikiwa hautapata matokeo mazuri,
Fanya maana kiko ndani ya uwezo wako kukifanya,
Fanya pasipo kujali ni watu wangapi wanakubaliana nawe katika hilo unalotaka kulifanya, thamini mchango wa hao wachache wanaokuunga mkono kwakuwa ndiyo wenye mtazamo sawa na wako kwa sasa; fanya na hao wachache kupata matokeo makubwa, Bwana Yesu alitumia mitume 11 kuufikia ulimwengu wote kwa njili,
Fanya kwakuwa ni wewe ndiye unayetakiwa kufanya usisubiri mtu mwingine,
Fanya wewe kwani hakuna mwingine kama wewe,
Fanya kwasababu yako mwenyewe na si kwa kuwafurahisha wengine, fanya ili ufurahie maisha yako,
Fanya sasa usingoje kesho, fanya kama hamna kesho, fanya leo kama kesho hautaishi,
Fanya na endelea kufanya, usijali hata wasipokushukuru sasa, yawezekana leo hawaoni faida ya hicho unachokifanya, faida ipo wataiona baadae na kukushukuru, kama si wao basi vizazi vyao,
Fanya tena, kusudia kufanya vizuri zaidi na kwa ubora wa kipekee,
Fanya makubwa na si ya kawaida yanayoweza kufanywa na mtu yeyote,
Fanya, una kila kitu kukuwezesha kufanya,
Fanya usijali kwamba eti hauna uzoefu,
Fanya hata vikwazo vikija tafuta njia ya kuvitatua huku ukiendelea kufanya,
Fanya kwa ujasiri; fanya tena, endelea kufanya, fanya tu hadi furaha yako ikamilike,
 
Rafiki yako,
Lazaro JP Kavageme