UMASKINI WA WATOTO
Umaskini
sio kitu cha lazima katika jumla nzima ya maisha ya mwanadamu, ni hali ya
ukosefu wa mahitaji ya msingi katika maisha ya mwanadamu kwa wakati, kwa mfano
mlo kamili, miundo mbinu ya maji safi na salama, mavazi, na miundombinu ya
habari na mawasiliano. Umaskini ni duru na hali ya kunaswa; umaskini wenyewe
una matawi manne, umaskini Kiroho, Kiuchumi, Kimwili, na Kijamii.
o
Kiroho;
umaskini kiroho ni hali ya kukosa uhusiano sahihi na Mungu, na kukosa kuwa na njia
ya uhakika kuishinda dhambi na kutokuwa na tumaini la uhakika kupata uzima wa
milele.
o
Kiuchumi;
umaskini kiuchumi ni ahali ya kukosa njia endelevu ya kujipatia mahitaji ya
msingi ya maisha.
o
Kimwili;
umaskini kimwili ni hali ya mwili ya kuwa katika dhiki, kuishi ama kuwepo
katika mazingira yasiyo rafiki kwa afya ya mwili, kuugua magonjwa
yanayoepukika, na hata kifo.
o
Kijamii;
umaskini kijamii ni hali ya mtu kukubali mazingira duni na kujiona ya kwamba
hana jinsi ya kuyabadili mazingira hayo na kuyatumia kuboresha maisha yake.
Umaskini wa Watoto na
vyanzo vyake:
Vipo
vyanzo mbalimbali vya umaskini wa Watoto. Mapambano dhidi ya umaskini na
jitihada za kuwatoa Watoto kwenye umaskini uliokithiri vinahitaji uelewa sahihi
na mkamilifu wa vyanzo vya umaskini huo, japo vyanzo vyenyewe baadhi yake ni
vigumu kudhaniwa ama kubainika.
- Uzalishaji usiowiana na idadi ya walaji:
Kulingana
na viwango vya uzalishaji, inaonekana kuwa katika nchi nyingi watu wanofanya
kazi za kujenga ni asilimia ndogo sana ukilinganisha na walaji. Tena kasi ya
kukua kwa uchumi ni ya chini ukilinganisha na kasi ya ongezeko la watu. Katika nchi kama Tanzania ambapo 51% yao ni
Watoto na vijana chini ya miaka 18, inaonekana kwamba wanaofanya kazi kuzalisha
ni wachache lakini watu wote wanakula hicho hicho kinachozalishwa na hao
wachache. Bado wanawake ndio hufanya kazi za uzalishaji kwa kiasi kikubwa kwa kilimo cha jembe la mkono na bila kufuata
kanuni za kilimo bora, zisizoleta uzalishaji unaohitajika kwa idadi ya Watoto.
Hali hii inaendeleza umaskini.
- Matumizi mabaya ya mali, hasa fedha na mazao ya chakula:
Angalia!
Watu walio wegi katika umaskini huwa na kasumba ya kutapanya fedha ama mazao
waliyoyapata kwa wingi, ulevi na kuoa wanawake zaidi. Hali hii yamkini hutokana
na kukosa uelewa wa kupanga vizuri kutumia vema mazao ama fedha zao; watu huwa
na mtazamo wa msimu badala ya kuwa na mtazamo wa muda mrefu, kwa hiyo watu
huchukulia kuwa vitu walivyo navyo ni vya msimu husika. Hata misemo ya
Kiswahili “ponda mali kufa kwaja”, vunja mifupa angali meno yapo” nk
- Uchumi mkubwa:
Mara
nyingi mifumo ya kiuchumi inawapuuza Watoto kabisa, ukuaji wa uchumi unaweza
kuongeza ugumu kwa mtu aliye katika umaskini. “Mpangilio wa uchumi katika miaka
ya 1990, ulimaanisha kuwa Watoto walihitaji kwa haraka sana sehemu yao katika
mafanikio ya Ulimwengu kwa kuwa wao ndio wenye uwezekano mdogo kabisa kunufaika
na mafanikio”. {Kofi Annan; katibu wa zamani Umoja wa Mataifa}.
- Uchangiaji wa gharama:
Kuchangia gharama za msingi kama vile afya na
elimu zina athali kwa vile zinagusa kwa nguvu zaidi ngazi ya familia na hivy
okuzidisah ugumu zaidi wa watu waishio katika umaskini.
- Uchumi wa mpito:
Lakini
pia mabadiliko ya hali ya maisha kutokana na mabadiliko ya sera na mfumo,
huenda yakafika akiwa yamechelewa na kukuta uwezekano wa Watoto kuondokana na
umaskini umekwisha kupita.
- Ubinafsishaji:
September
2002, Shirika la kuhudumia Watoto la SAVE THE CHILIDREN FUND, lilieleza kuwa kule kujihusisha kwa sekta
binafsi katika kutoa huduma za msingi, kuna uwezekano wa kuwa na matokeo mabaya
dhidi ya usawa na katika kupambambana na umaskini wa Watoto na kutimiza haki
zao. Pia kutokana na ubinafsishaji na muelekeo wa kupanua secta binafsi,
watumishi wengi wenye sifa na mafunzo yanayostahili walitoka kwenye secta ya
umma, madhara yalikuwa ni kudorora kwa secta hiyo, huku Watoto walio katika
umaskini wakiathiriwa zaidi.
- Siasa na utawala:
Mazingira
ya kisiasa na utawala yana uhusiano muhimu wa ustawi na maendeleo ya Watoto.
Mazingira ya siasa na utawala yenye utulivu, amani, na mshikamano huruhusu
huduma msingi za maisha kupatikana ipasavyo; mazingira ya siasa yenye vurugu na
utengano huleteleza fitina na Watoto
ndio wenye kubeba ukatili wa madhara ya vita.
- Mazingira:
Maumbile
ya mazingira ambapo Watoto wanaiishi {kijiogafia ama hali ya hewa}, huchangia
kuongeza ama kupunguza ukali wa maumivu ya umaskini. Watoto wanaozaliwa katika
mazingira fulani wana uwezekano mkubwa zaidi wa kupata lishe duni, wakati wale
wa mkoa mwingne wanapata lishe stahiki
kwazababu ya hali ya hewa na vipengele vingine vya mazingira.
- VVU na UKIMWI:
Haipaswi
kusahaulika kuwa afya, usalama na kupona kwa Watoto wote katika nchi zote
zilizoathiliwa, yanakwamishwa na matokeo ya UKIMWI juu ya familia na jamii.
Inakadiriwa kuwa hadi kufikia mwaka 2020, Watoto milioni 106 chini ya umri wa
miaka 15 kote duniani watakuwa wamepoteza mzazi mmoja ama wote wawili, huku
Watoto milion 25 kuwa yatima kutokana VVU na UKIMWI: Barani Afrika, idadi ya
yatima itaongezeka kufikia milioni 42, huku hapa Tanzania katika kila Watoto 8
chini ya miaka 15 mmoja atakuwa yatima, na zaidi ya nusu ya yatima wote
watakuwa ni kwa sababu ya UKIMWI. Hali ya Watoto kuwa yatima inasababisha
mazingira ya uhitaji mkubwa zaidi bila kuwa na msaada wa kufaa na wa uhakika:
ugonjwa huu unapunguza uzalishaji katika kazi za kuajiriwa, biashara, na
kilimo, na hivyo kudhoofisha mifumo ya kimaendeleo katika jamii: hii
inaendeleza umaskini kwa Watoto.
Mwisho:
Maumivu
ya umaskini humfanya mtu aliye katika umaskini ajione kwamba ameachwa bila
msaada wowote na kwamba hakuna anayemjali wala mwenye uwezo wa kumsaidia, kwa
maana hiyo umaskini ni kanusho la Upendo na Rehema za Mwenyezi Mungu kwa
maskini.
Vyanzo
vya umaskini wa watoto, kama tulivyoona hapo hapo juu ni vitu ama mazingira
yanayoepukika. Tunaweza kukomesha umaskini huu ikiwa kila mmoja atachukua hatua
kujiepusha na vitendo pamoja na kuepusha mazingira yanayopelekea hali
zinazoleta na kuendeleza umaskini wa watoto.
Social Plugin