"Baadhi yetu ni nafsi zilizokomaa sana kiasi kwamba hatukuja duniani ili tuwe tegemezi wa msaada wa wengine, bali tulikuja kuwa nguzo ya msaada kwa watu wengi". Ikiwa maisha yako yamekuwa na changamoto nyingi na unahisi hukuwahi kupata upendo au msaada wa kutosha, huenda ni kwa sababu wewe mwenyewe umeitwa kuwa chanzo cha upendo na msaada kwa wengine.
Wakati mwingine huenda mambo mema yasitokee kwako kwa sababu wewe ndiye jambo jema linalowatokea watu wengine. Ikiwa umewahi kuhisi kwamba unatoa kila ulicho nacho, unajitokeza kusaidia watu, unawabeba wengine, unajitahidi kubaki imara, lakini huoni mema yakikurudia, huenda hiyo ndiyo sababu.
Unaona.... wewe mwenyewe ni baraka. Namna unavyopenda, unavyolinda wengine, unavyowekeza katika maisha yao, na unavyodumu katika tabia njema hata unapokuwa umechoka—ndiyo inayowapa wengine nguvu ya kuendelea. Huenda si kwamba umesahaulika; huenda umeumbwa ili kuacha alama yenye maana katika maisha ya wengine. Hata hivyo hii isikuzuie kabisa kupokea msaada kutoka kwa watu unapouhitaji, hao ni kama wale kunguru waliotumwa kumlisha Eliya.
1 Wafalme 17:6
Social Plugin